Najua wengi wetu uwa tunajikuta kwenye wakati mgumu pindi linapo kuja suala la kupangilia rangi sahihi ya vazi tunalo vaa, ama mchanganyiko wa rangi tofauti tofauti.
Wengi wetu huaribu muonekano huu pindi tuanapo kuwa hatuelewi ni rangi ipi ambayo itafaa kuendana na rangi nyengine.
Hebu leo nizungumzie nguo zenye muoneka wa rangi kali ama zimezoeleka kwa jina la crazy color
TIPS ZITAKAZO KUSAIDIA KATIKA KUCHANGANYA RANGI
1.Kwanza unatakiwa kufahamu rangi ipi ambayo itaenda kutawala katika vazi lako kama ni hot pink ,njano,blue ama zambarau.
2. Vile vile hiyo rangi inatakiwa iendane na vito ambavyo utaenda kuvaa kama vile ,mkufu wenye rangi kali , hereni zenye rangi kali , pochi yenye rangi kali na viatu pia.
3. Makeup , katika kukamilisha muonekano wako wa makeup jaribu kupaka rangi zenye kuonekana kama vile, wanja rangi ya zambarau na lip gloss yenye rangi ya hot pink.
4. Kua makini sana katika namba ya rangi ambazo utachanganya itakua ni vizuri zaidi kama utachanganya
rangi kuanzia tatu hadi nne , lakini endapo utachanganya rangi nyingi zaidi itakua ni kichekesho kwa mfano mchanganyiko wa rangi tano hadi kuendelea.
Endapo utazingatia hayo haito kua shida katika kuchanganya rangi mbali mbali zenye muonekano mkali , na la muhimu zaidi ni kujua rangi yako ya mwili , kama ni mweusi sana basi ni bora uka punguza rangi ya nguo unazo enda kuchanganya , na kama ni mweupe unaweza ukatumia rangi zenye uwingi wowote.
No comments:
Post a Comment